Quantcast
Channel: Kamanda wa Matukio OnlineTv
Viewing all 21576 articles
Browse latest View live

*DAR ES SALAAM KUMEKUCHA, RAIS MAGUFULI ASHUSHA NEEMA.*

$
0
0

Wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam wameendelea *kula Matunda* ya serikali ya awamu ya tano baada ya *Rais Dr. John Magufuli* kutoa zaidi *Shilingi Billion 250* kwaajili ya utekelezaji wa *Miradi Mkakati* ya *kuziwezesha Halmashauri* za jiji hilo *kujiendesha zenyewe* ili kupunguza *utegemezi* wa fedha kutoka Serikali kuu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Paul Makonda* amesema miongoni mwa *miradi* itakayotekelezwa ni pamoja na *ujenzi wa kituo cha kisasa cha Mabasi ya Mikoani Mbezi Luis* kitakachogharimu zaidi ya shilingi *Billion 50* ambacho ujenzi wake utaanza *Mwezi June* na kuchukuwa *miezi 18* kukamilika.
*RC Makonda* amesema jengo hilo litakuwa na *gorofa tano* ambapo kituo hicho cha kisasa kitakuwa na uwezo wa kuchukuwa *Mabasi 200* na Maegesho *magari 300* (Underground parking) ambapo ndani kituo kutakuwa na huduma zote muhimu ikiwemo *Hotel, Hostel, Shopping Mall,Maduka, Migahawa, sehemu za mapumziko, Kituo cha Polisi, Bustani, Bank, Vyoo* vya kisasa pamoja na *Ofisi za kampuni za Magari.*
Aidha *RC Makonda* amesema miradi mingine ni Ujenzi wa *Soko la kisasa Kisutu* litakalogharimu shilingi *Billion 16*, Kituo cha Mabasi *Chamanzi Mkondogwa*, Ujenzi wa *Machinjio ya kisasa Vingunguti* yenye thamani ya *Billion 8.5* itakayokuwa na uwezo wa kuchinja *Ng'ombe 1,000* kwa siku hali itakayoondoa *uagizwaji wa Nyama Nje ya nchi* kwaajili ya kuuzwa kwenye *Hotel na Supermarket* ambapo kukamikika kwa mradi huu utawezesha *wazawa kupata soko la nyama la uhakika*, Ujenzi wa *Soko la Mburahati Billion Billion 2.7 kituo cha Daladala Tuangoma, Soko la Kibada Billion 14* pamoja na *miradi mingine mingi* ikiwemo *Fukwe za Coco, Ujenzi wa Shopping Mall* na miradi mingine lukuki inayofanywa na *Rais Magufuli* kwenye Mkoa wa Dar es salaam.
*RC Makonda* amemshukuru *Rais Magufuli* kwa kwa dhamira njema ya kusaidia *kutatua kero za wananchi* ambapo amewasihi wananchi wa Dar es salaam kukaa *mkao wa kula* kwa kuchangamkia *fursa za ajira* zitakazotolewa kwenye *miradi* hiyo.
*HUU NI UPENDO WA DHATI WA RAIS MAGUFULI KWA WANANCHI WAKE.*
Image may contain: sky and outdoor

NI KWELI MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMAAA!!!!!

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 11.05.2018

$
0
0


Mohammed SalahHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMohammed Salah
Mshambulijai wa Liverpool Mohamed Salah anasema kuwa hataondoka katika klabu hiyo mwisho wa msimu huu. Raia huyo wa MIsri mwenye umri wa miaka 25 amehusishwa na uhamisho wa kuelekea Real Madrid (Mirror)
Kiungo wa kati wa Ivory Coast Yaya Toure, 34, atakataa maombi kutoka China na mashariki ya kati kuendelea kucheza kwa kiasi kidogo cha fedha katika ligi ya Uingereza wakati atakapoondoka Manchester City mwisho wa msimu huu. (Mail)
Sergio Aguero
Image captionSergio Aguero
Manchester City inaongoza katika kutaka kumsajili kiungo wa kati wa Napoli Jorginho. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 raia wa Itali pia anasakwa na timu sita bora za ligi ya Uingereza.. (Times)
Atletico Madrid inataka kumsaini mshambuliaji Sergio Aguero kutoka Manchester City. Raia huyo mwenye umri wa miaka29- aliondoka Madrid 2011. (Mail)
Alvaro MorataHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionAlvaro Morata
Everton inaandaa dau la £25m kumnunua beki wa Newcastle na nahodha wake Jamaal Lascelles, 24. (Mirror)
Mkufunzi wa timu ya Uingereza Gareth Southgate anapima kumshirikisha beki wa Liverpool Trent Alexander-Arnold, 19, na winga wa Fulham Ryan Sessegnon, 17, katika kikosi chake cha wachezaji 35 cha kombe la dunia (Telegraph)
Juventus inajiandaa kuwasilisha ombi la £15m kwa klabu ya Chelsea ili kumnunua mshambuiliaji Alvaro Morata, 25, kwa mkopo. (Express)
MalcolmHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMalcolm
Liverpool inamnyatia winga wa Brazil na Bordeaux Malcom, 21. (Mail)
Klabu mpya iliopandishwa katika ligi kuu ya Uingereza Wolves imemuorodhesha wa kwanza katika usajili wake mshambuliaji wa AC Milan na Ureno Andre Silva mwisho wa msimu huu.
Andre SilvaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionAndre Silva
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 anadaiwa kugharimu £33m. (Sun)
Wolves inajiandaa kuwasilisha ombi la £30m kumsajili kipa wa Sporting Rui Patricio, 30, huku mchezaji huyo wa Ureno pia akisakwa na Napoli.(Diario de Noticias, via Birmingham Mail)
Carlos Carvahal
Image captionCarlos Carvahal
Swansea huenda ikamsajili meneja mwenye umri wa mdogo kuchukua mahala pake Carlos Carvahal baada ya ukufunzi wa Brendan Rodgers na Roberto Martinez. (Telegraph)
Mshambulaji wa Bournemouth Jermain Defoe amesema kuwa yeye mchezaji mwenza wa Uingereza Wayne Rooney walikuwa wamechoshwa na kombe la dunia la 2010 World hadi wakalazimika kutazama harusi ya Rooney katika DVD. (ESPN)
Winga wa Manchester City Leroy Sane
Image captionWinga wa Manchester City Leroy Sane
Miondoko ya densi ya Winga wa Manchester City Leroy Sane wakati wa ushindi wa kombe la ligi ilimtia wasiwasi mkufunzi Pep Guardiola, ambaye alisema kuwa kuwa aliogopeshwa na kiwango cha mchezaji huyo mwenye umri wa (Manchester Evening News)
Kipa wa Manchester City Ederson ameshinda rekodi ya dunia ya Guinness kwa kupiga mpira kwa urefu wa mita 75.35 (FourFourTwo)
Kungo wa kati wa Manchester United anyestaafu Michael Carrick anasema kuwa mkufunzi Alex Ferguson alikuwa akimchezesha wakati wa mvua. (ESPN)

Eric Cantona kurudi Old Trafford

$
0
0


Eric CantonaHaki miliki ya pichaUNICEF
Mchezaji wa zamani wa Manchester United na Ufaransa Eric Cantona anatarajiwa kurudi katika uwanja wa OLd Trafford mnamo mwezi Juni.
Atacheza katika uwanja wa Manchester United katika mechi ya hisani ya shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watoto Unicef.
Raia huyo mwenye umri wa miaka 51anasema kuwa: Hakuna mahali pazuri kama nyumbani .
Kujua kwamba nitarudi katia uwanja wa OLd Trafford ni hisia maalum.Atajiunga na idadi kubwa ya watu maarufu duniani akiwemo Usain Bolt na mO Farah , Olly Murs na Gordon Ramsay.
Eric CantonaHaki miliki ya pichaUNICEF
Image captionEric Cantona
Cantona atashiriki katika kikosi cha wachezaji 11 maarufu kitakachoshirikisha wachezaji wa zamani na watu maarufu wakiongozwa na nahodha Usain Bolt.
Itakuwa mara ya kwanza kwa yeye kucheza katika uwanja huo tangu 2001.
''Ninarudi kuhakikisha kuwa mechi hiyo ya Juni 10 ndio bora zaidi na nataka mujiunge nami'', alisema raia huyo wa Ufaransa.
"Njooni tuweke historia katika uwanja wa OLd Trafford kwa mara nyengine ya mwisho''.
Atakabiliana na kikosi cha Uingereza kitakachoongozwa na mwanzilishi wa soka ya hisani Robbie Williams.
Sir Mo Farah na Usain BoltHaki miliki ya pichaUNICEF
Image captionMo Farah na Usain Bolt kukabiliana katika mechi ya Unicef OLd Trafford
Atajiunga na wachezaji wengine wa zamani wa Manchester United akiwemo Phil Nevile na Edwin van der Sar.
Wachezaji wengine wa kikosi hicho cha dunia watakuwa Yaya Toure, Clarence Seedorf, Robert Pires , Jaap Stam na Patrick Kluivert.
Watakabiliana na David Seaman, Jamie Redknapp, Danny Murphy na Robbie Fowler kwa upande wa kikosi cha UIngereza.
Cantona ambaye alijiunga na klabu ya Manchester United kwa dau la £1.2m in 1992 - alifunga mabao 64 katika mechi 143 za ligi akiichezea Manchester United na kushinda mataji manne ya ligi ya Uingereza pamoja na mataji mawili ya kombe la FA katika misimu mitano.
Lakini jezi yake nambari saba pia ilikumbwa na utata hususan wakati alipompiga teke shabiki mmoja wakati wa mechi.Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionLakini jezi yake nambari saba pia ilikumbwa na utata hususan wakati alipompiga teke shabiki mmoja wakati wa mechi.
Lakini jezi yake nambari saba pia ilikumbwa na utata hususan wakati alipompiga teke shabiki mmoja wakati wa mechi.
Alipigwa marufuku kwa miezi minane kwa kisa hicho cha 1995. Tangu astaafu katika soka 1997, Cantona amekuwa akiigiza katika filamu ikiwemo ile ya Elizabeth, French Film na Looking for Eric.

WEWEEE KAMANDA

Sheria ya uhalifu wa kimitandao Kenya: Kenyatta aidhinisha sheria inayotoa adhabu ya dola 50,000 kwa habari feki

$
0
0


Haki miliki ya pichaPSCU
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameidhinisha Mswada wa Sheria za Uhalifu wa Kompyuta na Mtandaoni wa 2018 kuwa Sheria, hatua itakayotoa adhabu kali kwa watakaopatikana na makossa ya mtandaoni.
Sheria hiyo inatoa adhabu ya faini ya Sh5 milioni (dola 50,000 za Marekani) au kifungo cha miaka miwili jela, au adhabu zote mbili, kwa atakayepatikana na kosa la uenezaji wa habari za uzushi.
Mtu atakayepatikana na kosa la kueneza taarifa ambazo zinaweza kuzua taharuki au kuzua vurugu atafungwa jela zaidi ya miaka kumi.
Sheria hiyo inatarajiwa kuathiri utendakazi wa wanahabari, vyombo vya habari, watumiaji wa mitandao ya kijamii, wanablogu na watu wengine wanaotumia kompyuta na mitandao.

Lakini je ni kweli sheria hiyo mpya itakandamiza uhuru wa kujieleza?

Wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa wanahabari mapema mwezi huu, mwenyekiti wa Chama cha Wahariri Kenya Bw Churchill Otieno alikuwa amesema sheria hiyo inaweza kutumiwa kuminya uhuru wa wanahabari.
Alieleza kuwa kifungu kinachozungumzia uenezaji wa habari za uzushi au uongo kinaweza kutumiwa vibaya na maafisa wa dola.
Je ni kweli sheria mpya ya Uhalifu wa Mtandao itakandamiza uhuru wa kujieleza Kenya ?
Kiongozi wa zamani wa Chama cha Wanasheria Kenya Apollo Mboya amenukuliwa na vyombo vya habari akisema kifungu hicho kinaweza kuwapa watawala 'uhuru' wa kukandamiza vyombo vya habari.
Shirika la kimataifa la kutetea uhuru wa wanahabari Committee to Protect Journalists (CPJ) nalo lilikuwa limemhimiza Rais Kenyatta kutoidhinisha mswada huo kuwa sharia.
Makundi ya kueteta haki za binaadamu wameishutumu sheria hiyo na kuitaja kuwa ya hatari.
Shirika la Article 19 East Africa, linataja makosa kadhaa yalio mapana ambayo yana adhabu kali zinazoweza mwishowe kuzuia uhuru wa kujieleza katika mitandao Kenya.
Haki miliki ya pichaReuters
Image caption Makundi ya kueteta haki za binaadamu wameishutumu sheria hiyo na kuitaja kuwa ya hatari.
Sheria hiyo bado inawacha wazi masuala kadhaa, kama vile kusambazwa kwa picha za utupu kwa dhamira ya kumchafulia mtu jina, udukuzi, na utumiaji haramu wa data binafsi - licha ya kushutumiwa pakubwa shughuli za kampuni ya Cambridge Analytica katika uchaguzi mara mbili wa urais nchini.

Daktari ashtakiwa kuiba moyo wa marehemu Kenya

$
0
0
Mkuu wa zamani wa uchunguzi wa chanzo cha vifo Kenya ameshtakiwa kosa la kuiba moyo kutoka kwenye maiti iliyokuwa inafanyiwa upasuaji.
Dkt Moses Njue alikanusha shtaka hilo aliposomewa mashtaka katika mahakama ya Hakimu Mkuu Nairobi.
Dkt Njue alikuwa ameshtakiwa kwamba yeye, pamoja na mwanawe, Lemuel Anasha Mureithi, ambaye hakuwepo kortini na ambaye alikuwa mchunguzi msaidizi wake.
Walidaiwa kuiba moyo wa Timothy Mwandi Muumbo wakifanyia mwili wake upasuaji 25 Juni, 2015 katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Lee Funeral Home.
Hakimu Mkuu Francis Andayi aliagiza Bw Mureithi afike mahakamani na kujibu mashtaka kabla ya kesi kuanza kusikizwa 3 Julai.
Dkt Njue alikanusha pia shtaka jingine la kuuharibu moyo ili kuficha ushahidi , akifahamu kwamba ripoti ya uchunguzi wa maiti hiyo ingetumiwa kwenye kesi iliyokuwepo kortini.
Alishtakiwa pia kosa la tatu la kuuondoa moyo huo kutoka kwenye maiti bila idhini, kosa ambalo pia alilikanusha.
Mahakama ilikuwa awali imekataa ombi la Dkt Njue la kuahirisha kusomewa kwa mashtaka akisema jamaa zake Muumbo walikuwa wamewasilisha kesi jingine Mahakama ya Kuu kumtaka kuutoa moyo huo.
Dkt Njue alikuwa amesema kesi hiyo itaingilia kesi hiyo iliyo Mahakama Kuu.
Lakini Hakimu Andayi alikubaliana na upande wa mashtaka na kusema hakuna msingi wowote wa kuzuia kesi hiyo iliyokuwa mbele yake kuendelea.
Dkt Njue aliachiliwa kwa dhamana ya Sh300,000 (dola 3,000 za Marekani) pesa taslimu.
Kesi hiyo imeanza siku chache baada ya familia nyingine kudai ililazimika kuzika mwili wa jamaa wao ukiwa bila moyo baada ya Dkt Njue kufanya upasuaji kuchunguza chanzo cha kifo chake.
Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Kenya alikuwa amependekeza Dkt Njue, aliyejiuzulu miaka kadha iliyopita kuanzisha chuo chake cha mafunzo ya utabibu ashtakiwe kwa wizi wa viungo vya Benedict Karau.
Bw Karau, kutoka Meru mashariki mwa jiji la Nairobi alifariki mnamo 2 Machi, 2015 kwa njia isiyoeleweka.

Utafiti: Malazi ya Sokwewatu ni masafi kuliko ya binaadamu

$
0
0

Malazi ya Sokwe mtu ni masafi kuliko ya binaadam, wanasayansi wamebaini. Viumbe hawa hujenga malazi kwa kutumia matawi na majani ya miti ambapo hulala.
Malazi ya sokwe mtu ni mfano kwa mwanadamu kijana ambaye anaweza kuona vigumu kufuata
Mwanafunzi wa Marekani wa shahada ya Uzamivu Megan Thoemmes, aliyeongoza jopo kukusanya sampuli za uchafu kutoka kwenye Sokwe watu 41 katika bonde la Issa nchini Tanzania: ''Tunajua kuwa makazi ya binaadamu yana aina mbalimbali ya viumbe.
''Mfano, takriban asilimia 35 ya vijidudu kwenye vitanda vya binaadamu vinatoka kwenye miili yetu wenyewe, ikiwemo, kinyesi, kinywani na vijidudu vya kwenye ngozi
''Tulitaka kujua ni kwa namna gani hali hii inaweza kufananishwa na Sokwe hawa,ambao huandaa vitanda vyao kila siku.
Sokwe mzee zaidi kwenye hifadhi afariki Marekani
Kumbe sokwe sio wapenzi wa muziki
Ikilinganishwa na vitanda vya binaadamu, sehemu za kulala ya sokwe zilikuwa na aina mbalimbali za wadudu, matokeo ambayo hayakutarjiwa katika misitu ya kitropiki
Haki miliki ya pichaLwiro Primates and Anthony Caere
Hata hivyo,uwezekano ni mdogo sana kwa sokwemtu kupata ''uchafu'' kinyesi, kinywa au bakteria kwenye ngozi.
''Hatukuona vijidudu kwenye malazi ya Sokwe mtu, jambo lililoshangaza kidogo'', alieleza Bi Thoemmes kutoka Chuo cha North Carolina .
Walishangazwa na walichokigundua walipojaribu kusafisha malazi ya hao chimpanzee kuondosha viroboto na chawa waliokuwepo.
Watafiti wanasema vitanda vya Sokwe watu ni visafi zaidi kuliko vya binaadamu, ingawa viumbe hawa hutumia zaidi ya nusu siku kitandani.
Wanasayansi wamegundua kuwa malazi ya Sokwewatu nchini Tanzania yana kiasi kidogo cha kinyesi na bakteria kuliko magodoro ya binaadamu majumbani, kwa sababu viumbe hawa huhama malazi kila usiku.

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 16.05.2018

$
0
0
Haki miliki ya pichaReuters
Image caption Mauricio Pochettino
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino yuko tayari kuwakataa Chelsea kwa sababu anasema ana furaha kuwa na klabu yake. (Star)
Arsenal wamefanya mazungumzo na kiungo wa kati wa Nice Jean-Michael, 26, ambaye thamani yake ni pauni milioni 40. Lakini mahasimu wao wa London Chelsea wanaongoza mbio na kumsaini raia huyo wa Ivory Coast. (Mirror)
Kiungo wa kati wa Arsenal Mikel Arteta, 36 anakaribia kuwa meneja mpya wa Arsenal akichukua nafasi ya Arsene Wenger baada ya mazungumzo kuendelea kati ya pande hizo mbili. (Independent)
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Mikel Arteta
Nahodha wa zamani wa Arsenal Patrick Vieira, 41, anasema amekasirishwa mshahara ulionukuliwa na klabu hiyo baaada ya kuzungumziwa kuhusu nafasi ya umeneja iliyo wazi. (Sky Sports)
Manchester United wana uhakika wa kumsaini mlinzi Toby Alderweireld, 29, kutoka Tottenham. Red Devils wana nia ya kutumia pauni milioni 40 kwa mchezaji huyo wa kimataifa raia wa Ubelgiji. (Evening Standard)
United pia wako kwenye mazungumzo ya kumsaini beki Matthew Bondswell, 16, kutoka Nottingham Forest. (Mail)
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Harry Maguire
Mlinzi wa Leicester Harry Maguire, 25, hatma yake itaamuliwa baada ya mechi za kombe la dunia baada vilabu kadha vikuu vya Premier League kummezea mate mechezaji huyo wa kimataifa wa England. (Mirror)
Everton watahitaji kulipa pauni milioni 6 ikiwa watamfuta meneja Sam Allardyce. Menajwea wa zamani wa Watford Marco Silva ndiye ana nafasi nzuri ya kuchukua wadhifa huko Goodison Park. (Express)
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Marco Silva
Liverpool watamsaini kiungo wa kati Isaac Christie-Davies, 20, baada ya mchezaji kutopewa mkataba mpya huko Stamford Bridge. (ESPN)
QPR watamateua meneja wa zamani wa England Steve McClaren kama meneja wao mpya kuchukua mahala pake Ian Holloway, ambaye alifutwa wiki iliyopita. (Sky Sports)
BORA ZAIDI KUTOKA JUMANNE
Kiungo wa kati wa Newcastle Jonjo Shelvey, 26, hatajumuishwa kwenye kikosi cha Uingereza kitakachoshiriki kombe la dunia kutokana rekodi yake mbaya kinidhamu. (Mirror)
Manchester United wako tayari kuilipa Napoli pauni milioni 44 kumpata beki Elseid Hysaj msimu huu. Raia huyo wa Albania wa umri wa miaka 24 atakuwa mlinzi namba saba ghalia zaidi duniani. (Sun)
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Sam Allardyce
Everton watamfuta meneja Sam Allardyce saa 48 zinazokuja na wanakaribia kumteua aliyekuwa meneja wa Watford Marco Silva. (Mirror)
Afisa mkuu mtendaji wa Arsenal Ivan Gazidis na mkrugeni mkuu Josh Kroenke wamemtambua kiungo wa kati wa zamani wa Arsenal Mikel Arteta ambaye sasa ni kocha huko Manchester City kama mtu anayeweza kuchukua mahala pake Arsene Wenger kama meneja wa Arsenal. (Mail)

Article 6

$
0
0
Brazil wamemtaka mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar, ambaye bado anauguza jeraha, katika kikosi cha wachezaji 23 ambao wanatarajiwa kuchezea taifa hilo katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi.
Neymar, 26, alifanyiwa upasuaji mwezi Machi na daktari wa timu ya taifa ya Brazil alisema hataweza kucheza kwa miezi mitatu.
Wachezaji wanne wanaochezea Manchester City Ederson, Danilo, Fernandinho na Gabriel Jesus ni miongoni mwa wachezaji wanaosakatia gozi Ligi ya Premia ambao wamo kwenye kikosi hicho.
Wengine ni nyota wa Liverpool Roberto Firmino na winga wa Chelsea Willian.
Beki wa kulia wa PSG Dani Alves atakosa michuano hiyo baada ya kupata jeraha la goti wiki iliyopita.
Brazil wamo Kundi E na Costa Rica, Serbia na Uswizi na watacheza mechi yao ya kwanza Jumapili 17 Juni.
Kikosi kamili cha Brazil:
Walinda lango: Alisson (Roma), Ederson (Manchester City), Cassio (Corinthians).
Mabeki: Danilo (Manchester City), Fagner (Corinthians), Marcelo (Real Madrid), Filipe Luis (Atletico Madrid), Thiago Silva, Marquinhos (both PSG), Miranda (Inter Milan), Pedro Geromel (Gremio).
Viungo wa kati: Casemiro (Real Madrid), Fernandinho (Manchester City), Paulinho (Barcelona), Fred (Shakhtar Donetsk), Renato Augusto (Beijing Guoan), Philippe Coutinho (Barcelona), Willian (Chelsea), Douglas Costa (Juventus).
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Neymar ndiye mchezaji aliyenunuliwa ghali zaidi duniani
Washambuliaji: Neymar (PSG), Taison (Shakhtar Donetsk), Gabriel Jesus (Manchester City), Roberto Firmino (Liverpool).

CHADEMA YATOA MAPINGAMIZI NANE KESI YA UCHOCHEZI

$
0
0

UPANDE WA UTETEZI KESI YA 'UCHOCHEZI' INAYOWAKABILI VIONGOZI CHADEMA WATOA MAOMBI YAO ,WAWASILISHA MAPINGAMIZI NANE

Na Karama Kenyynko,Blogu ya jamii

UPANDE wa utetezi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe, wameomba Mahakama kutupilia mbali mashtaka dhidi ya washtakiwa kwa kuwa yanamapungufu, kisheria.

Maombi hayo yamewasilishwa leo mahakamani hapo  mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Wilabard Mashauri wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Wakili Peter Kibatala.Hivyo amewasilisha mapingamizi nane ya kisheria yanayoshambulia uhalali wa hati ya mashtaka na mashtaka dhidi ya washtakiwa.

Katika mapingamizi hayo, Kibatala amedai, kibali cha DPP kina mapungufu ya kisheria kwa sababu haioneshi imetolewa kwa mashtaka yapi  na pia hati ya mashtaka imewataja majina washtakiwa wote bila ya kufafanua na pia imetaja tu kifungu cha sheria ambacho washtakiwa wameshtakiwa nacho 
Amedai, hakuna kibali kilichowasilishwa mahakamani hapo kwa maana hiyo mashtaka dhidi ya washtakiwa yamepelekwa mahakamani hapo bila ridhaa ya DPP.

Amedai Aidha Kibatala ametoa ombi mbadala na kuomba, iwapo Mahakama itashindwa kuifuta hati nzima ya mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao basi iyafutilie mbali mashtaka ambayo yanamapungufu kisheria. Ikiwamo shtaka la nne, latano, la sita na la saba.

Alidai, maelezo ya mashtaka hayo yanawachanganya washtakiwa na hawawezi kujitetea ipasavyo. Pia mashtaka hayo kufunguliwa kwake kunahitaji ridhaa ya (DPP) ambayo haipo kutokana na mapungufu hayo, inaonesha hakuna ridhaa yake.

Amebainisha kwa kuwa mashtaka hayo tajwa kufunguliwa kwake kunahitaji ridhaa ya DPP, lakini kuwa haipo tunaomba yafutiliwe mbali. Alidai Kibatala.Pia alidai hati ya mashtaka inamapungufu kwa sababu shtaka la pili na la Tatu hayana maelezo ya kutosheleza ya kuwapa washtakiwa msingi na uwezo wa kuweza kujitetea kikamilifu katika kesi hiyo ya jinai.

Alidai, katika shtaka la kufanya mkusanyiko bila kibali hati haijataja watu waliotishiwa na wametajwa kwa wingi hivyo haijulikani ni washtakiwa ama ni watu wengine.

Akiendelea kuwasilisha maoungamizi hayo, kibatala amedai, mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao yamejichanganya na hayaonyeshi walipelekeaje kifo cha Akwilina na hao majeruhi walijeruhiwa na nani na kwa kutumia nini.

Amedai, maelezo katika hati ya mashtaka yamerundikana  kiasi kwamba ni vigumu mtu kujitetea na kwamba unapomshtaki mtu  kwa kisababisha kifo ni lazima utoe Maelezo ya kutosha kuonesha unamaanisha kitu Fulani ili mtu  aweze kujitetea.

Pia amedai mapungufu mengine yaliyomo kwenye hati hiyo ni kuwa hayaoneshi dhumuni la pamoja ambalo washtakiwa walikutana kulitenda hivyo linawanyang'anya washtakiwa haki ya kujitetea.

Kibatala alidai kuwa hati ya mashtaka inamapungufu kwa sababu  vifungu vilivyotajwa katika shtaka la Tatu, tano na saba siyo sahihi.

Alidai katika shtaka la 10,11 na 12 yanamapungufu kisheria kwa sababu hayaonyeshi watu waliochochewa kufanya makosa ni wakina nani waliohudhuria mkutano, wakazi wa kinondoni ama wapiga kura bila kujali itikadi zao.

AJIBU MAPIGO 

Wakili wa Serikali Mkuu,Paul Kadushi ameiomba Mahakama kuyatupilia mbali mapingamizi yote hayo ya upande kwa kuwa hayana mashiko kisheria. Kuhusu kibali cha DPP kinachoipa Mahakama ridhaa ya kusikiliza kesi,Kadushi amedai hakuna uamuzi wowote ulioweka msingi kwamba ni lazima kiwepo na nini ama hakipaswi kuwepo na nini.

Mbali na  Mbowe wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo Namba 112 ya 2018 ni  mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika.

Mbunge wa Tarime mjini Esterher Matiko, Katibu wa chama hicho Dk  Vicenti  Mashinji na mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na  mbunge wa bunda, Esther Bulaya.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na jumla ya mashtaka 12 katika kesi ya jinai namba 112 ya mwaka 2018 ikiwamo kula njama, kufanya mkusanyiko usio halali kinyume cha sheria na kuendelea kufanya mkusanyiko usio halali ama maandamano yaliyosababisha kifo cha Akwilina.

WAKUU WA MIKOA KANDA YA ZIWA VICTORIA WAKOSOA VIKALI TABIA YA WANASIASA KUIPAKA MATOPE DHAMIRA NJEMA YA SERIKALI KUPAMBANA NA UVUVI HARAMU

$
0
0


NA JOHN MAPEPELE, MWANZA

WAKUU wa mikoa inayozunguka Ziwa Victoria wamekosoa vikali tabia ya baadhi ya wanasiasa kuipaka matope dhamira njema ya Serikali ya kupambana na uvuvi haramu ulioshamiri katika ziwa hilo na kutaka viongozi wa aina hiyo kutangaza masilahi yao kwenye eneo la uvuvi kabla ya kuwashambulia viongozi wanaosimamia zoezi hilo kwa misingi ya kisheria.

Wakizungumza kwenye kikao cha tathmini ya operesheni sangara awamu ya  pili iliyowahusisha Wakuu wa Mikoa,Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Makamanda wa Polisi wa mikoa na Wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wa mikoa yote inayozunguka Ziwa Victoria jijini Mwanza jana viongozi hao wametaka hatua zaidi zichukuliwe ili kunusuru rasilimali hizo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka alielezea kuchukizwa na tabia inayoanza kuota mizizi ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kuipaka matope dhamira nzuri ya Serikali ya kukabiliana na uvuvi haramu na kutaka viongozi wa aina hiyo watangaze masilahi yao kabla ya kuanza kuwashambulia viongozi wanaosimamia operesheni hiyo inayotekelezwa kwa mujibu wa sheria .
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akihutubia  hadhara ya kikosi kazi cha watu 260 alichokiunda kwa ajili ya operesheni Sangara 2018 na Wakuu wa Mikoa mitano inayozunguka Ziwa vicktoria  wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni  hiyo. Picha na John Mapepele
  Viongozi wakuu wa Wizara  ya  Mifugo na Uvuvi waliokaa  wakiwa katika picha ya pamoja na makamanda wakuu wa Operesheni Sangara 2018 (waliosimama) wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni  hiyo. 

“Viongozi wanaopinga operesheni ya kupambana na uvuvi haramu ni muhimu watangaze kwanza masilahi yao kuhusu eneo la uvuvi ili wasiendelee kuchafua taswira za viongozi wanaosimamia wizara hii”alisema Mtaka.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela alisema kumekuwepo na dhana zinazojengeka kwamba viongozi wa mikoa inayozunguka Ziwa Victoria hawaungi mkono mapambano ya kukabiliana na uvuvi haramu operesheni jambo ambalo alisema ni upotoshaji mkubwa na kwamba Serikali ya mkoa iko mstari wa mbele na kuwabana watendaji wa ngazi zote watakaobanika kufadhili uvuvi haramu.

Alisema ni muhimu operesheni hiyo iwe endelevu na kubainisha kuwa suala la uvuvi haramu haliwezi kumalizika kama hakuna dhamira ya dhati miongoni mwa wasimamizi wa sheria na kwamba uongozi wa mkoa huo hautakubali kuendelea kuwa na watumishi wazembe wataoshindwa kusimamia suala hilo.

Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina alitangaza kuanza kwa awamu ya tatu ya Operesheni Sangara yenye lengo la kupambana na uvuvi haramu katika Ziwa Victoria sambamba na kutangaza operesheni katika maziwa yote na kuagiza viongozi wakuu wa mikoa na wilaya kuwachukulia hatua kali viongozi wa chini wanaobanika kujihusisha na kufadhili uvuvi haramu.
Viongozi wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi waliokaa wakiwa katika picha ya pamoja na sekretarieti ya Operesheni Sangara 2018 (waliosimama) wakati wa mkutano wa kufanya tathimini ya Operesheni hiyo. 

Pia alitangaza kuunda kanda mpya ya udhibiti na usimamizi rasilimali za uvuvi katika wilaya za Ukerewe na Sengerema huku akiunda ofisi mpya ya Kanda jijini Mwanza itakayokuwa inaratibu shughuli zote katika kanda hizo saba ili kuongeza usimamizi madhubuti wa rasilimali hizo.

Aidha Mpina aliongeza kuwa katika awamu ya tatu ya operesheni hiyo itahusisha pia Mahakama zinazotembea ili kuweza kutoa hukumu huko huko ziwani hali itayowezesha kuondokana kabisa na uvuvi haramu.

Aidha aliwataka watu wote wanaopinga operesheni ya uvuvi haramu wasome takwimu ili kujua ukubwa wa tatizo katika Ziwa Victoria ambapo jumla ya watuhumiwa 3,284 wamekamatwa kujihusisha na uvuvi haramu huku samaki wasioruhusiwa kilo 326,751 , mabondo kilo 5,142 zilikamatwa zikitoroshwa kwenda nje ya nchi na nyavu haramu 566,497 nazo zilikamatwa na kuteketezwa. Pia magari 257, mitumbwi 1278 , pikipiki 269 na injini za mitumbwi 564 vilikamatwa vikihusishwa na makosa ya uvuvi haramu.

Alisema katika baadhi ya maeneo ya Bushengere wilayani Ukerewe wazazi wamewaonya watoto wao kutotumika na mafisadi kwenye uvuvi haramu kwani wakikamatwa wao ndio wanaopata tabu na kutelekezwa ambapo wameweka azimio la kukataa kutumika tena kwenye jambo hilo.

Alisema kutokana na operesheni hizo zinazoendelea za kupambana na uvuvi haramu hadi kufikia mwezi Disemba mwaka huu watu wote wanaopinga na hata kuwaombea mabaya viongozi wa operesheni watapata aibu kubwa kwani idadi ya samaki itaongezeka huku akitoa wito kwa viongozi wa ngazi zote wenye mapenzi mema na nchi kuunga mkono vita hiyo kwa manufaa ya Taifa.

Katibu Mkuu Uvuvi, Dk. Yohana Budeba alisema wizara hiyo imejipanga kikamilifu kuhakikisha sekta ya uvuvi inatoa mchango mkubwa katika pato la Taifa na kwamba operesheni hiyo itaendelea hadi pale uvuvi haramu utakapokoma.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Tano Mwera alisema wamekuwa wakipokea malalamiko mengi kuhusu operesheni hiyo lakini kila walipofuatilia kupata ushahidi wa malalamiko hayo waliukosa jambo ambalo wamebaini kuwa ni njama za makusudi za kutaka kuhujumu nia njema ya Serikali ya kupambana na kutokomeza uvuvi haramu.

Kamanda Mkuu wa operesheni hiyo kutoka Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Hassan Shelukindo alisema katika operesheni hiyo jumla ya watuhumiwa 22 wakiwemo wenyeviti wa vijiji na vitongoji na viongozi wa BMU wamefungwa  jela huku wengine 17 mashauri yao yakiwa yanaendelea Mahakamani kwa makosa ya kujihusisha na uvuvi haramu.

Shelukindo alisema pia watumishi 6 walikuwa kwenye operesheni hiyo waliondolewa kwa makosa mbalimbali ikiwemo ukiukwaji wa maadili ya kazi ambapo watumishi hao watachukuliwa hatua za kinidhamu na taasisi zao huku jumla ya sh. bilioni 7.5 zikikusanywa kutokana na faini pamoja mauzo ya mabondo,samaki na kayabo.

DC SHINYANGA AZINDUA RASMI ZOEZI LA KUGAWA VITAMBULISHO VYA TAIFA KWA WANANCHI

$
0
0


Uzinduzi huo umefanyika leo Jumatano Mei 16,2018 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo katika ofisi za Manispaa ya Shinyanga. Mkuu huyo wa wilaya amekabidhi vitambulisho 12,918 kwa maafisa watendaji wa kata 17 za manispaa hiyo watakaokwenda kugawa vitambulisho hivyo kwa wananchi. 

“Hapa nchini, hili ni zoezi la kwanza la ugawaji vitambulisho kwa wananchi kwa kutumia ugawaji wa mkupuo,tunaanzia katika manispaa ya Shinyanga,nakabidhi rasmi vitambulisho hivi kwa maafisa watendaji wa kata ambao watagawa vitambulisho kwa wananchi”,alieleza Matiro. 

Aidha aliwataka maafisa watendaji kuwa makini na kugawa vitambulisho hivyo haraka huku akisisitiza kuwa vitambulisho hivyo havitolewi kwa ubaguzi bali kila mwananchi ana haki ya kupata. 

“Zoezi kujiandikisha linaendelea katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga lakini kwa upande wa manispaa ya Shinyanga tumemaliza zoezi la uandikishaji kinachoendelea sasa ni kugawa vitambulisho,hili ni zoezi endelevu wale ambao hawajiandikisha wafike katika ofisi za NIDA kujiandikisha ili wapate vitambulisho”,aliongeza Matiro. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,Mratibu wa NIDA mkoa wa Shinyanga Nathanael Fredrick Njau alisema tangu waanze zoezi la uandikishaji mwezi Septemba 2017 katika manispaa ya Shinyanga wamezalisha jumla ya vitambulisho 17,780 na tayari wameshagawa vitambulisho 3651 kwa watumishi wa umma na leo vitambulisho 12,918 kwa wananchi na zoezi la uandikishaji na ugawaji vitambulisho linaendelea. 

Naye Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi NIDA Makao makuu,Stephen Kapesa aliwasisitiza wananchi ambao bado hawajisajili waendelee kujisajili katika ofisi za Uhamiaji huku akiwataka kutoa ushirikiano kuwafichua watu wasiostahili kupata vitambulisho hivyo. 

“Uzalishaji wa vitambulisho unaendelea na tunatarajia hadi mwezi Desemba mwaka huu kila mwanachi awe na kitambulisho,NIDA inaomba wananchi kufichua watu wasiotahili kupata vitambulisho hivi wakiwemo wahamiaji haramu”,aliongeza Kapesa. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi aliwataka maafisa watendaji kutoendekeza urasimu katika ugawaji wa vitambulisho na hatarajii kusikia kitambulisho cha mwananchi kimepotea. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa zoezi la kugawa vitambulisho vya taifa (NIDA) kwa wananchi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga. Kushoto ni Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Agnes Machiya. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi NIDA Makao makuu,Stephen Kapesa - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa zoezi la kugawa vitambulisho vya taifa (NIDA) kwa wananchi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akiwasisitiza maafisa watendaji wa kata kuwa makini katika zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wananchi ili kuepuka changamoto inayoweza kujitokeza ya kupotea kwa vitambulisho.
Mratibu wa NIDA mkoa wa Shinyanga Nathanael Fredrick Njau akisoma taarifa ya zoezi la uandikishaji na utoaji vitambulisho vya taifa katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi NIDA Makao makuu,Stephen Kapesa akizungumzia kuhusu zoezi la utoaji vitambulisho vya taifa.
Maafisa watendaji,madiwani na watumishi mbalimbali wa manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi la ugawaji vitambulisho.
Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Agnes Machiya akimkaribisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kuzindua rasmi zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya taifa kwa wananchi wa manispaa ya Shinyanga.
Sehemu ya vitambulisho 12,918 vilivyokabidhiwa kwa maafisa watendaji wa kata 17 za manispaa ya Shinyanga watakaokwenda kugawa vitambulisho hivyo kwa wananchi. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akimkabidhi Kitambulisho cha taifa Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Agnes Machiya wakati akizindua rasmi zoezi la kugawa vitambulisho vya taifa (NIDA) kwa wananchi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi akionesha kitambulisho chake cha taifa baada ya kukabidhiwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akimkabidhi Kitambulisho cha taifa diwani wa kata ya Lubaga Mchungaji Obedi Jilala (CHADEMA).
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akimkabidhi Kitambulisho cha taifa diwani wa viti Maalum Manispaa ya Shinyanga Mariam Nyangaka (CCM).
Diwani wa kata ya Kizumbi,Reuben Kitinya akipokea kitambulisho cha taifa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akikabidhi Vitambulisho vya taifa kwa afisa mtendaji wa kata ya Mwawaza,Nhiga Nhiga ili akavigawe kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akikabidhi Vitambulisho vya taifa kwa afisa mtendaji wa kata ya Ndembezi,Felister Msemelwa ili akavigawe kwa wananchi wa kata hiyo.
Mratibu wa NIDA mkoa wa Shinyanga Nathanael Fredrick Njau akisisitiza jambo wakati wa zoezi la ugawaji vitambulisho vya taifa kwa maafisa watendaji wa kata za manispaa ya Shinyanga.
Maafisa watendaji na madiwani wakiwa ukumbini.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

MOI SASA KUFANYA UPASUAJI KWA WAGONJWA 1000 KWA MWEZI ASEMA MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN.

$
0
0

NA WAMJW-DAR ES SALAAM

TAASISI ya Mifupa nchini MOI sasa itafanya upasuaji wa mifupa kwa wagonjwa wapatao 1000 kwa mwezi kutoka wagonjwa 500 mpaka 700 baada ya kupokea msaada wa chumba cha upasuaji na vifaa vyake kutoka kwa Serikali ya Kuwait .

Hayo yamesemwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa kuzindua na kupokea msaada wa chumba cha upasuaji na vifaa vyake vyenye thamani ya shilinigi milioni 186 leo katika Taasisi ya mifupa MOI leo jijini Dar es salaam.

“Hii ni faraja kubwa sana kwa Serikali kwani uboreshwaji wa huduma katika hospitali zetu za kibingwa kubwa kama MOI itaweza kuhudumia wagonjwa wengi Zaidi kutoka wagonjwa 700 kwa mwezi mpaka kufikia 1000 kwa mwezi” alisema Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Aidha Makamu wa Rais Samia Suluhu amesema kuwa anaishukuru Serikali ya Kuwait kupitia Balozi wake Jasem Al Najem kwa msaada huo kwani utaisaidia kwa kiasi kikubwa MOI katika kuboresha utoaji huduma hasa katika fani ya upasuaji kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi hapa nchini.

Kwa uapnde wake Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa kukamilika kwa vyumba hivi viwili vya upasuaji, kutaiwezesha Taasisi ya MOI kuwa na jumla ya vyumba vya upasuaji 8 kutoka 6 vilivyopo sasa na miongoni mwa vyumba hivi vya upasuaji kimoja kitakuwa maalumu kwa ajili ya watoto tu.

“MOI imeshatoa matibabu ya upasuaji kwa wagonjwa 1,670 ikiwemo upasuaji mifupa (wagonjwa 1,228), kubadilisha nyonga (wagonjwa 84), kubadilisha goti (wagonjwa 72), upasuaji wa uti wa mgongo (wagonjwa 109), ubongo (wagonjwa 64), na watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi (wagonjwa 113” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuimarisha na kuboresha afya za Watanzania jengo hilo pia litakuwa na vitanda 16 vya ICU (Intensive Care Unit) na 16 vya HDU (High Dependency Unit), hivyo kuimarisha huduma za tiba kwa wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.

Naye Balozi wa Kuwait Nchini Balozi Jasem Al Najem amesema kuwa Nchi ya Kuwait ipo mstari wa mbele katika kuhakikisha Hospitali na Vituo vya afya nchini Tanzania vinatoa huduma bora za Afya kwa kutumia Taaluma na ujuzi wa kisasa ikiwemo vifaa na vifaa tiba .

“Serikali ya Kuwait itakuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika kuimarisha afya za wananchi kwa kuendelea kutoa misaada mbalimbali ikiwemo vifaa,vifaa tiba na wataalamu wa afya na kutochoka katika hilo” alisema Balozi Najem.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MOI Bi. Zakia Mejhi amesema kuwa Taasisi yake imeokoa Bilioni 3 za kufanyia upasuaji kwani kwa sasa huduma hizo za kibingwa zinafanyika nchini kwa Shilingi Bilioni 12 kutoka Bilioni 15 za rufaa ya kwenda kutibiwa nje.

Elimu ya Mlipa Kodi Kutolewa Mashuleni

$
0
0


Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Serikali imeona umuhimu wa kuingiza elimu ya mlipa kodi kwenye mitaala ya elimu nchini ili kwajengea Watanzania tabia, mwenendo na mazoea ya kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa.

Kauli hiyo imetolewa leo, Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Lupembe Mhe. Joram Ismael Hongoli juu ya kwa nini Serikali isiingize kwenye mitaala ya elimu somo la umuhimu wa kulipa kodi ili lifundishwe kuanzia shule ya msingi ili wananchi wapate uelewa wa kodi na waweze kulipa kodi kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea.

"Serikali inatambua umuhimu wa elimu ya mlipa kodi katika kumjengea mwananchi tabia ya kulipa kodi. Katika somo la Uraia na Maadili kuanzia darasa la III na kuendelea, mtaala umelenga kumjengea na kumuandaa mwanafunzi kuwa mwajibikaji katika kutekeleza majukumu ya kila siku," alisema Mhe. Ole Nasha.

Vile vile mtaala umelenga kumjengea mwanafunzi kuiheshimu na kuithamini jamii yake kwa kuwa mwadilifu na mzalendo ikiwa ni pamoja na kutekeleza majukumu ya kitaifa ikiwemo kulipa kodi.

Aidha amesema, kutokana na umuhimu wa kuwajengea vijana utamaduni wa kulipa kodi, elimu ya mlipa kodi ni jambo muhimu, Serikali kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikisha Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) itaendelea kuboresha elimu hiyo ili isisitizwe na kuwekewa mkazo katika mitaala ya elimu kuanzia elimu ya Msingi.

Wakati huo huo, Mhe. Ole Nasha amesema Serikali ilifuta ada na michango ya lazima katika shule za umma ngazi ya elimu ya msingi (elimu ya awali hadi kidato cha Nne) na mpango huo hakuhusisha kidato cha tano na sita pamoja na shule binafsi.

Ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Seter Alexander Mahawe juu ya lini, Serikali itafuta ada kwa wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi.

"Ada na michango iliyokuwa inalipwa na wazazi/walezi kwa sasa hugharamiwa na Serikali. Mpango huu haukuzihusu shule binafsi pamoja na shule za Umma ngazi ya kidato cha Tano na Sita. Hivyo shule hizo zitaendelea na utaratibu wa wazazi/walezi kuchangia gharama za uendeshaji wa elimu ikiwemo kulipa ada za mitihani.

Hata hivyo amesema, Ili kuhakikisha mazingira rafiki katika utoaji wa elimu, Serikali imekuwa ikifanya majadiliano na sekta binafsi kwa lengo la kuondoa changamoto zinazowakabili ambapo hadi sasa Serikali imeweza kuondoa baadhi ya kodi na tozo mbalimbali ambazo awali walikuwa wakitozwa wamiliki wa shule binafsi.

Ametoa mfano wa kodi hizo kuwa ni kodi za mabango, kodi ya kuendeleza ufundi standi stadi (Skills Developmentt Levy), tozo ya Afya na Usalama mahala pa kazi (Occupational Safety and Health Administration - OSHA) na tozo ya zimamoto.

WAMACHINGA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA KUJISAJILI NA KUPATIWA VITAMBULISHO MAALUM

$
0
0


Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (katikati) akizindua usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Wa pili kushoto ni Meneja wa TRA Mkoa wa Arusha Bw. Faustine Mdessa.
Kiongozi wa Kikundi cha Levolosi Machinga Group Bw. Hassan Shayo maarufu kama G akikabidhiwa kitambulisho wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitabulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (wa tatu kulia) akiwa ameketi meza kuu wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.
Baadhi ya wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi baada ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao ulioandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.(PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO


Na Veronica Kazimoto,Arusha,

Wito umetolewa kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi hususani wamachinga kujisajili na hatimaye kupatiwa vitambulisho maalum kwa lengo la kusaidia biashara zao kutambulika, kukopesheka na kurahisisha mawasiliano ya usimamizi wa biashara hizo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo uliofanyika leo mkoani Arusha, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Fabian Daqqaro amesema ni muhimu wafanyabiashara kutumia fursa hii ya kujisajili ili kurasimisha biashara zao.
“Ni matumaini yangu kuwa, wafanyabiashara wengi wadogo wadogo mkoani hapa, mtatumia fursa hii kujisajili kwa sababu ninafahamu wengi wenu malengo yenu siyo kuwa wafanyabiashara wadogo muda wote, bali mtakuza biashara zenu na kuwa wafanyabiashara wakubwa na hii itawezesha kuchangia mapato ya Serikali,” alisema Daqqaro.
Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Kodi za Ndani kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Abdul Zuberi ameeleza kuwa, zoezi hili la kuwasajili na kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara wadogo limetokana na juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
“Ni ukweli usiopingika kwamba, Rais wetu kwa nyakati tofauti amekuwa akiwapigania na kutaka wafanyabiashara wadogo wadogo kutambulika rasmi na kupatiwa vitambulisho ikiwa ni pamoja na kutafutiwa maeneo rafiki ya kufanyia biashara zao,” alisema Zuberi.
Ameongeza kuwa, kutokana na juhudi hizo za Rais Magufuli, Serikali kupitia Kikao cha Bunge la Bajeti la Mwaka wa Fedha 2017/2018, ilifanya marekebisho mbalimbali ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 ambapo moja ya marekebisho hayo ni kuwatambua na kuwapatia vitambulisho maalum wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi na jukumu hili limekasimiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Zuberi alisema kuwa, zoezi hili limeshafanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam na Mwanza na sasa limefanyika mkoani Arusha ambapo jumla ya vikundi 125 vya wafanyabiashara wadogo vinatarajiwa kusajiliwa na hadi sasa vikundi 25 vimeshatambuliwa vikiwa na jumla ya wafanyabiashara wadogo takribani 3,600 na kwa uwakilishi wafanyabiashara 100 wamepatiwa vitambulisho jijini hapa.
Naye Kiongozi wa Wamachinga mkoani Arusha Fredson Athumani, ameishukuru Serikali kwa kuwatambua rasmi na kusisitiza kuwa, atahakikisha anashirikiana na viongozi wenzake pamoja na Serikali kuwahamasisha wafanyabiashara wote wadogo kusajiliwa na kupata vitambulisho maalumu.
Zoezi la usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi linafanyika chini ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Serikali za Mitaa, Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) pamoja na Idara ya Uhamiaji.

Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 18.05.2018

$
0
0


Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Mikel Arteta
Kiungo wa kati wa zamani wa Arsenal Mikel Arteta, 36, anakaribia kuchukua mahala pake Arsene Wenger huko Emirates. (Daily Telegraph)
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola na mkurugenzi wa kandanda Txiki Begiristain wamempa ruhusa naibu kocha Arteta kuzungumza na klabu yake ya zamani. (Sport)
Arsenal pia wana nia ya kuzungumza na Thierry Henry kuhusu nafasi ya umeneja iliyo wazi mapema wiki ijayo. (Sky Sports)
Haki miliki ya pichaRex Features
Image caption Rafael Benitez
Rafael Benitez, anayeaminiwa kutafutwa na West Ham atachagua kubaki kama maneja wa Newcastle lakani anataka kuhakikishiwa kuhusu bajeti ya kununua wachezaji kutoka mmiliki wa klabu Mike Ashley. (Daily Telegraph)
Benitez anataka pauni milioni 100 za kununua wachezaji kuwa mwamuzi mkuu kuhusu kuwanunua wachezaji na mshahara wa pauni milioni 6 kwa mwaka ili kuweza kusalia huko St James' Park. (Daily Express)
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Gianluigi Buffon
Liverpool wanataka kipa raia wa Italia Gianluigi Buffon, 40, ambaye amaendoka Juventus baada ya miaka 17, lakini huenda wakakabiliwa na ushindani kutoka Manchester City. (Sun)
Juventus wanataka kurudisha Alvaro Morata ambaye alichezea klabu hiyo kati ya mwaka 2014 na 2016. Mchezaji huyo wa miaka 25 alifunga magoli 11 katika mechi 31 za Premier League wakati wa msimu wake wa kwanza huko Chelsea. (Independent)
Haki miliki ya pichaRex Features
Image caption Alvaro Morata
Chelsea wamekana kuamruhusu mchezaji wa mkopo Michy Batshuayi, 24, kujiunga na Borussia Dotmund, lakini wanakaribisha klabu hiyo ya Ujerumani kumsaini Morata. (Daily Mirror)
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero, 29, anasema anatarajia tu kucheza na nyota wa Barcelona Lionel Messi katika kikosi cha Argentina, anasema ama afura kuwa huko Etihad. (Corriere dello Sport in Italian)
Haki miliki ya pichaEmpics
Image caption Sergio Aguero
Ajenti wa kiungo wa safu ya kati wa Napoli Jorginho anasema mchezaji huyo atahamia Manchester City ikiwa vilabu hivyo vitakubaliana kuhusu fedha. Napoli wanataka hadi pauni milioni 60 kwa mchezaji huyo wa miaka 26 lakini City wanataka wakubaliane kiwango kinachokaribia pauni milioni 50. (Manchester Evening News)
Napoli wametangaza euro milioni 120 kwa mchezaji wa kimataifa raia wa senegal Kalidou Koulibaly, 26, katika jaribio la kuzuia Real Madrid, Chelsea na Manchester United. (RAI Sport, via Football Italia)
Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Kalidou Koulibaly
Shakhtar Donetsk wametangaza kuwa kocha mkuu Paulo Fonseca - ambaye amehusishwa na West Ham na Everton amesaini mkataba wa miaka miwili. (Shakhtar Donetsk)
Leicester wamekubaliana pauni milioni 17.5 na Porto kwa mlinzi Ricardo Pereira, 24. (A Bola, via Leicester Mercury)
Klabu iliyoshindwa ya West Brom inatarajiwa kumtafuta meneja mpya wiki hii na inaweza kumgeukia kocha mkuu wa Brentford Dean Smith, 47. (London Evening Standard)
Mshambulizi wa Paris St-Germain Mbrazil Neymar, 26, amerejea mazoezi baada ya kupata jeraha mwezi Februari (Daily Mail)

Urusi 2018: Dembele, Pogba, Griezmann na Mbappe wajumuishwa kwenye kikosi cha Ufaransa Kombe la Dunia

$
0
0
Mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial na Alexandre Lacazette wa Arsenal wameachwa nje ya kikosi cha Ufaransa kitakachoshiriki Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka huu.
Martial, 22, ameshinda mataji 18 na kuanza katika kikosi kilichoshinda kwa mabao 3-1 wakati wa mechi ya kirafiki na Urusi mwezi Machi.
Lacazette, 26, alishinda taji la mwisho kati ya 16 wakati wa mechi ya kirafiki na Ujerumani mwezi Novemba.
Kiungo wa kati wa Marseille Dimitri Payet hayuko kwenye kikosi hicho cha Ufaransa.
Beki wa Manchester City Benjamin Mendy ni kati ya wachezaji wa Premier League walijuuishwa licha ya kurejea uwanjani mwezi Aprili baada ya karibu miezi ishirini kufuatia jeraha.
Kiungo wa kati wa Chelsea N'Golo Kante na mshambulizi Olivier Giroud, kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba na kipa wa Tottenham Hugo Lloris ni wachezaji wengine wanaosakata kabumbu England waliojumuishwa katika kikosi hicho cha wachezaji 23.



Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Anthony Martial na Alexandre Lacazette waachwa nje
Kiungo wa kati wa Stoke Steven N'Zonzi pia naye amejumuishwa.
Mshambuliaji wa Bayern Munich Kingsley Coman na kiungo wa kati wa Paris St-Germain Adrien Rabiot pia nao wameachwa nje.
Ufaransa wako kundi la C pamoja na Australia, Peru na Denmark.
Kikosi kamili cha Ufaransa:
Walinda Lango: Hugo Lloris (Tottenham Hotspur), Steve Mandanda (Marseille), Alphonse Areola (Paris Saint-Germain)
Walinzi: Lucas Hernandez (Atletico Madrid), Presnel Kimpembe (Paris Saint-Germain), Benjamin Mendy (Manchester City), Benjamin Pavard (Stuttgart), Adil Rami (Marseille), Djibril Sidibe (Monaco), Samuel Umtiti (Barcelona), Raphael Varane (Real Madrid)
Viungo wa kati: N'Golo Kante (Chelsea), Blaise Matuidi (Juventus), Steven N'Zonzi (Sevilla), Paul Pogba (Manchester United), Corentin Tolisso (Bayern Munich)
Washambuliaji: Ousmane Dembele (Barcelona), Nabil Fekir (Lyon), Olivier Giroud (Chelsea), Antoine Griezmann (Atletico Madrid), Thomas Lemar (Monaco), Kylian Mbappe (Paris Saint-Germain), Florian Thauvin (Marseille)

Mada zinazohusiana

Wachezaji watakaocheza Kombe la Dunia 2018 Urusi

$
0
0
Wachezaji watakaowakilisha mataifa yote 32 yanayoshiriki Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi mwaka huu kadiri wanavyotangazwa.
BBC tutakupasha kadiri wachezaji wanavyotangazwa.

Kundi A

Russia (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Igor Akinfeev (CSKA Moscow), Vladimir Gabulov (Club Brugge), Soslan Dzhanaev (Rubin Kazan), Andrey Lunev (Zenit St Petersburg).
Mabeki: Vladimir Granat, Ruslan Kambolov, Fedor Kudryashov (wote wa Rubin Kazan), Ilya Kutepov (Spartak Moscow), Roman Neustadter (Fenerbahce), Konstantin Rausch (Dynamo Moscow), Andrey Semenov (Akhmat Grozny), Igor Smolnikov (Zenit St Petersburg), Mario Fernandes (CSKA Moscow).
Viungo wa kati: Yuri Gazinskiy (Krasnodar), Alexsandr Golovin, Alan Dzagoev (both CSKA Moscow), Aleksandr Erokhin, Yuri Zhirkov, Daler Kuzyaev (wote wa Zenit St Petersburg), Roman Zobnin, Alexsandr Samedov (wawili wa Spartak Moscow), Anton Miranchuk (Lokomotiv Moscow), Aleksandr Tashaev (Dynamo Moscow), Denis Cheryshev (Villarreal).
Washambuliaji: Artem Dzyuba (Arsenal Tula), Aleksey Miranchuk (Lokomotiv Moscow), Fedor Smolov (Krasnodar), Fedor Chalov (CSKA Moscow).

Saudi Arabia

Bado kikosi hakijatangazwa
Misri(Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Essam El Hadary (Al Taawoun), Mohamed El-Shennawy (Al Ahly), Sherif Ekramy (Al Ahly), Mohamed Awad (Ismaily).
Mabeki: Ahmed Fathi, Saad Samir, Ayman Ashraf (all Al Ahly), Mahmoud Hamdy (Zamalek), Mohamed Abdel-Shafy (Al Fateh), Ahmed Hegazi (West Brom), Ali Gabr (Zamalek), Ahmed Elmohamady (Aston Villa), Karim Hafez (Lens), Omar Gaber (Los Angeles FC), Amro Tarek (Orlando City).
Viungo wa kati: Tarek Hamed, Mahmoud Abdel Aziz (both Zamalek), Shikabala (Al Raed), Abdallah Said (KuPS), Sam Morsy (Wigan Athletic), Mohamed Elneny (Arsenal), Kahraba (Al Ittihad), Ramadan Sobhi (Stoke City), Trezeguet (Kasimpasa), Amr Warda (Atromitos Athens).
Washambuliaji: Marwan Mohsen (Al Ahly), Ahmed Gomaa (Al Masry), Kouka (Braga), Mohamed Salah (Liverpool).
Uruguay (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Fernando Muslera (Galatasaray), Martin Silva (Vasco da Gama), Martin Campana (Independiente).
Mabeki: Diego Godin (Atletico Madrid), Sebastian Coates (Sporting Lisbon), Jose Maria Gimenez (Atletico Madrid), Maximiliano Pereira (Porto), Gaston Silva (Independiente), Martin Caceres (Lazio), Guillermo Varela (Penarol).
Viungo wa kati: Nahitan Nandez (Boca Juniors), Lucas Torreira (Sampdoria), Matias Vecino (Inter Milan), Federico Valverde (Real Madrid), Rodrigo Bentancur (Juventus), Carlos Sanchez (Monterrey), Giorgian De Arrascaeta (Cruzeiro), Diego Laxalt (Genoa), Cristian Rodriguez (Penarol), Jonathan Urretaviscaya (Monterrey), Nicolas Lodeiro (Seattle Sounders), Gaston Ramirez (Sampdoria).
Washambuliaji: Cristhian Stuani (Girona), Maximiliano Gomez (Celta Vigo), Edinson Cavani (Paris St-Germain), Luis Suarez (Barcelona).

Kundi B

Ureno
Walinda lango: Anthony Lopes (Lyon), Beto (Goztepe), Rui Patricio (Sporting Lisbon)
Mabeki: Bruno Alves (Rangers), Cedric Soares (Southampton), Jose Fonte (Dalian Yifang), Mario Rui (Napoli), Pepe (Besiktas), Raphael Guerreiro (Borussia Dortmund), Ricardo Pereira (Porto), Ruben Dias (Benfica)
Viungo wa kati: Adrien Silva (Leicester), Bruno Fernandes (Sporting Lisbon), Joao Mario (West Ham), Joao Moutinho (AS Monaco), Manuel Fernandes (Lokomotiv Moscow), William Carvalho (Sporting)
Washambuliaji: Andre Silva (AC Milan), Bernardo Silva (Manchester City), Cristiano Ronaldo (Real Madrid), Gelson Martins (Sporting Lisbon), Goncalo Guedes (Valencia), Ricardo Quaresma (Besiktas)
Uhispania
Kikosi bado hakijatangazwa
Morocco
Walinda lango: Mounir El Kajoui (Numancia), Yassine Bounou (Girona), Ahmad Reda Tagnaouti (Ittihad Tanger)
Mabeki: Mehdi Benatia (Juventus), Romain Saiss (Wolves), Manuel Da Costa (Basaksehir), Badr Benoun (Raja Casablanca), Nabil Dirar (Fenerbahce), Achraf Hakimi (Real Madrid), Hamza Mendyl (LOSC)
Viungo wa kati: M'barek Boussoufa (Al Jazira), Karim El Ahmadi (Feyenoord), Youssef Ait Bennasser (Caen), Sofyan Amrabat (Feyenoord), Younes Belhanda (Galatasaray), Faycal Fajr (Getafe), Amine Harit (Schalke 04)
Washambuliaji: Khalid Boutaib (Malatyaspor), Aziz Bouhaddouz (Saint Pauli), Ayoub El Kaabi (Renaissance Berkane), Nordin Amrabat (Leganes), Mehdi Carcela (Standard de Liege), Hakim Ziyech (Ajax).
Iran (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Alireza Beiranvand (Persepolis), Seyed Hossein Hosseini (Esteghlal), Rashid Mazaheri (Zob Ahan), Amir Abedzadeh (Maritimo).
Mabeki: Ramin Rezaeian (Ostende), Voria Ghafouri (Esteghlal), Steven Beitashour (Los Angeles FC), Seyed Jalal Hosseini (Persepolis), Mohammad Reza Khanzadeh (Padideh), Morteza Pouraliganji (Alsaad), Mohammad Ansari (Persepolis), Pejman Montazeri, Seyed Majid Hosseini (both Esteghlal), Milad Mohammadi (Akhmat Grozny), Omid Norafkan (Esteghlal), Saeid Aghaei (Sepahan), Roozbeh Cheshmi (Esteghlal).
Viungo wa kati: Saeid Ezatolahi (Amkar Perm), Masoud Shojaei (AEK Athens), Ahmad Abdolahzadeh (Foolad), Saman Ghoddos (Ostersunds), Mahdi Torabi (Saipa), Ashkan Dejagah (Nottingham Forest), Omid Ebrahimi (Esteghlal), Ehsan Hajsafi (Olympiacos), Ali Karimi (Sepahan), Soroush Rafiei (Al Khor), Ali Gholizadeh (Saipa), Vahid Amiri (Persepolis).
Washambuliaji: Alireza Jahanbakhsh (AZ Alkmaar), Karim Ansarifard (Olympiacos), Mahdi Taremi (Al Gharafa), Sardar Azmoun (Rubin Kazan), Reza Ghoochannejhad (Heerenveen), Kaveh Rezaei (Charleroi).

Kundi C

Ufaransa
Walinda lango: Hugo Lloris (Tottenham Hotspur), Steve Mandanda (Marseille), Alphonse Areola (Paris Saint-Germain)
Mabeki: Lucas Hernandez (Atletico Madrid), Presnel Kimpembe (Paris Saint-Germain), Benjamin Mendy (Manchester City), Benjamin Pavard (Stuttgart), Adil Rami (Marseille), Djibril Sidibe (Monaco), Samuel Umtiti (Barcelona), Raphael Varane (Real Madrid)
Viungo wa kati: N'Golo Kante (Chelsea), Blaise Matuidi (Juventus), Steven N'Zonzi (Sevilla), Paul Pogba (Manchester United), Corentin Tolisso (Bayern Munich)
Washambuliaji: Ousmane Dembele (Barcelona), Nabil Fekir (Lyon), Olivier Giroud (Chelsea), Antoine Griezmann (Atletico Madrid), Thomas Lemar (Monaco), Kylian Mbappe (Paris Saint-Germain), Florian Thauvin (Marseille)
Australia (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Brad Jones (Feyenoord), Mitch Langerak (Nagoya Grampus), Mat Ryan (Brighton), Danny Vukovic (Genk).
Mabeki: Aziz Behich (Bursaspor), Milos Degenek (Yokohama F. Marinos), Alex Gersbach (RC Lens), Matthew Jurman (Suwon Samsung Blue Wings), Fran Karacic (NK Lokomotiva), James Meredith (Millwall), Josh Risdon (Western Sydney), Trent Sainsbury (Grasshopper Zurich), Aleksandar Susnjar (FK Mlada Boleslav), Bailey Wright (Bristol City).
Viungo wa kati: Josh Brillante (Sydney FC), Jackson Irvine (Hull City), Mile Jedinak (Aston Villa), Robbie Kruse (VfL Bochum), Massimo Luongo (QPR), Mark Milligan (Al-Ahli), Aaron Mooy (Huddersfield), Tom Rogic (Celtic), James Troisi (Melbourne Victory), Tim Cahill (Millwall).
Washambuliaji: Daniel Arzani (Melbourne City), Apostolos Giannou (AEK Larnaca), Tomi Juric (Luzern), Mathew Leckie (Hertha Berlin), Jamie Maclaren (Hibernian), Andrew Nabbout (Urawa Red Diamonds), Dimitri Petratos (Newcastle Jets), Nikita Rukavytsya (Maccabi Haifa).
Peru
Kikosi bado hakijatangazwa
Denmark (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Kasper Schmeichel (Leicester), Frederik Ronnow (Brondby), Jonas Lossl (Huddersfield), Jesper Hansen (FC Midtjylland).
Mabeki: Simon Kjaer (Sevilla), Andreas Bjelland (Brentford), Mathias Jorgensen (Huddersfield), Andreas Christensen (Chelsea), Henrik Dalsgaard (Brentford), Jannik Vestergaard (Borussia Monchengladbach), Jens Stryger Larsen (Udinese), Jonas Knudsen (Ipswich), Nicolai Boilesen, Peter Ankersen (both FC Copenhagen), Riza Durmisi (Real Betis).
Viungo wa kati: Christian Eriksen (Tottenham), Daniel Wass (Celta Vigo), Lasse Schone (Ajax Amsterdam), Lukas Lerager (Bordeaux), Mathias Jensen (Nordsjaelland), Michael Krohn-Dehli (Deportivo La Coruna), Mike Jensen (Rosenborg), Pierre-Emile Hojbjerg (Southampton), Thomas Delaney (Werder Bremen), William Kvist (FC Copenhagen).
Washambuliaji: Andreas Cornelius (Atalanta), Kasper Dolberg (Ajax), Kenneth Zohore (Cardiff City), Martin Braithwaite (Bordeaux), Nicklas Bendtner (Rosenborg), Nicolai Jorgensen (Feyenoord), Pione Sisto (Celta Vigo), Robert Skov, Viktor Fischer (both FC Copenhagen), Yussuf Poulsen (RB Leipzig).

Kundi D

Argentina (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Sergio Romero (Manchester United), Nahuel Guzman (Tigres Monterrey), Wilfredo Caballero (Chelsea), Franco Armani (River Plate).
Mabeki: Gabriel Mercado (Sevilla), Federico Fazio (Roma), Nicolas Otamendi (Manchester City), German Pezzella (Fiorentina), Ramiro Funes Mori (Everton), Marcos Rojo (Manchester United), Nicolas Taglafico (Ajax), Javier Mascherano (Hebei Fortune), Marcos Acuna (Sporting Lisbon), Eduardo Salvio (Benfica), Cristian Ansaldi (Torino).
Viungo wa kati: Ever Banega, Guido Pizarro (both Sevilla), Lucas Biglia (AC Milan), Leandro Paredes (Zenit St Petersburg), Angel Di María, Giovani Lo Celso (both Paris St-Germain), Enzo Perez (River Plate), Manuel Lanzini (West Ham), Pablo Perez, Cristian Pavon (both Boca Juniors), Maximiliano Meza (Independiente), Ricardo Centurion (Racing), Rodrigo Battaglia (Sporting Lisbon).
Washambuliaji: Lionel Messi (Barcelona), Gonzalo Higuain, Paulo Dybala (both Juventus), Mauro Icardi (Inter Milan), Sergio Aguero (Manchester City), Diego Perotti (Roma), Lautaro Martinez (Racing).
Iceland (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Hannes Halldorsson (Randers), Runar Alex Runarsson (Nordsjaelland), Frederik Schram (Roskilde).
Mabeki: Ari Freyr Skulason (Lokeren), Hordur Magnusson (Bristol City), Ragnar Sigurdsson (Rostov), Kari Arnason (Aberdeen), Holmar Orn Eyjolfsson (Levski Sofia), Sverrir Ingi Ingason (Rostov), Birkir Mar Saevarsson (Valur), Samuel Kari Fridjonsson (Valerenga).
Viungo wa kati: Gylfi Sigurdsson (Everton), Aron Gunnarsson (Cardiff City), Emil Hallfredsson (Udinese), Birkir Bjarnason (Aston Villa), Johann Berg Gudmundsson (Burnley), Olafur Ingi Skulason (Karabukspor), Arnor Ingvi Traustason (Malmo), Rurik Gislason (Sandhausen).
Washambuliaji: Alfred Finnbogason (Augsburg), Bjorn Bergmann Sigurdarson (Rostov), Jon Dadi Bodvarsson (Reading), Albert Gudmundsson (PSV Eindhoven).
Croatia (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Danijel Subasic (Monaco), Lovre Kalinic (Gent), Dominik Livakovic (Dinamo Zagreb), Karlo Letica (Hajduk Split).
Mabeki: Vedran Corluka (Lokomotiv Moscow), Domagoj Vida (Besiktas), Ivan Strinic (Sampdoria), Dejan Lovren (Liverpool), Sime Vrsaljko (Atletico Madrid), Josip Pivaric (Dynamo Kyiv), Tin Jedvay (Bayer Leverkusen), Matej Mitrovic (Club Brugge), Borna Barisic (Osijek), Zoran Nizic (Hajduk Split), Duje Caleta-Car (Red Bull Salzburg), Borna Sosa (Dinamo Zagreb).
Viungo wa kati: Luka Modric, Mateo Kovacic (both Real Madrid), Ivan Rakitic (Barcelona), Milan Badelj (Fiorentina), Marcelo Brozovic (Inter Milan), Marko Rog (Napoli), Mario Pasalic (Chelsea), Filip Bradaric (Hajduk Split).
Washambuliaji: Mario Mandzukic (Juventus), Ivan Perisic (Inter Milan), Nikola Kalinic (AC Milan), Andrej Kramaric (Hoffenheim), Marko Pjaca (Schalke), Ante Rebic (Eintracht Frankfurt), Duje Cop (Standard Liege), Ivan Santini (Caen).
Nigeria (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Ikechukwu Ezenwa (Enyimba), Daniel Akpeyi (Chippa United), Francis Uzoho (Deportivo Fabril), Dele Ajiboye (Plateau United).
Mabeki: William Ekong (Bursaspor), Leon Balogun (FSV Mainz), Olaoluwa Aina (Hull City), Kenneth Omeruo (Kasimpasa), Bryan Idowu (Amkar Perm), Chidozie Awaziem (Nantes), Abdullahi Shehu (Bursaspor), Elderson Echiejile (Cercle Brugge), Tyronne Ebuehi (Ado Den Haag), Stephen Eze (Lokomotiv Plovdiv).
Viungo wa kati:Mikel John Obi (Tianjin Teda), Ogenyi Onazi (Trabzonspor), Wilfred Ndidi (Leicester), Oghenekaro Etebo (Las Palmas), John Ogu (Hapoel Be'er Sheva), Uche Agbo (Standard Liege), Joel Obi (Torino), Mikel Agu (Bursaspor).
Washambuliaji: Ahmed Musa, Kelechi Iheanacho (both Leicester), Moses Simon (Gent), Victor Moses (Chelsea), Odion Ighalo (Changchun Yatai), Alex Iwobi (Arsenal), Junior Lokosa (Kano Pillars), Simeon Nwankwo (Crotone).

Kundi E

Brazil
Walinda lango: Alisson (Roma), Ederson (Manchester City), Cassio (Corinthians).
Mabeki: Danilo (Manchester City), Fagner (Corinthians), Marcelo (Real Madrid), Filipe Luis (Atletico Madrid), Thiago Silva, Marquinhos (both Paris St-Germain), Miranda (Inter Milan) Pedro Geromel (Gremio).
Viungo wa kati: Casemiro (Real Madrid), Fernandinho (Manchester City), Paulinho (Barcelona), Fred (Shakhtar Donetsk), Renato Augusto (Beijing Guoan), Philippe Coutinho (Barcelona), Willian (Chelsea), Douglas Costa (Juventus).
Washambuliaji: Neymar Jr (Paris St-Germain), Taison (Shakhtar Donetsk), Gabriel Jesus (Manchester City), Roberto Firmino (Liverpool).
Switzerland
Kikosi bado hakijatangazwa
Costa Rica (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Keylor Navas (Real Madrid), Patrick Pemberton (Liga Deportiva Alajuelense), Leonel Moreira (Herediano).
Mabeki: Cristian Gamboa (Celtic), Ian Smith (Norrkoping), Ronald Matarrita (New York City), Bryan Oviedo (Sunderland), Oscar Duarte (Espanyol), Giancarlo Gonzalez (Bologna), Francisco Calvo (Minnesota United), Kendall Waston (Vancouver Whitecaps), Johnny Acosta (Aguilas Dorados).
Viungo wa kati: David Guzman (Portland Timbers), Yeltsin Tejeda (Lausanne-Sport), Celso Borges (Deportivo La Coruna), Randall Azofeifa (Herediano), Rodney Wallace (New York City), Bryan Ruiz (Sporting Lisbon), Daniel Colindres, Christian Bolanos (both Saprissa).
Washambuliaji: Johan Venegas (Saprissa), Joel Campbell (Real Betis), Marco Urena (Los Angeles FC).
Serbia
Kikosi bado hakijatangazwa

Kundi F

Ujerumani (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Bernd Leno (Bayer Leverkusen), Manuel Neuer (Bayern Munich), Marc-Andre ter Stegen (Barcelona), Kevin Trapp (Paris St-Germain).
Mabeki: Jerome Boateng (Bayern Munich), Matthias Ginter (Borussia Monchengladbach), Jonas Hector (Cologne), Mats Hummels (Bayern Munich), Joshua Kimmich (Bayern Munich), Marvin Plattenhardt (Hertha Berlin), Antonio Rudiger (Chelsea), Niklas Sule (Bayern Munich), Jonathan Tah (Bayer Leverkusen).
Viungo wa kati: Julian Brandt (Bayer Leverkusen), Julian Draxler (Paris St-Germain), Leon Goretska (Schalke), Ilkay Gundogan (Manchester City), Sami Khedira (Juventus), Toni Kroos (Real Madrid), Mesut Ozil (Arsenal), Sebastian Rudy (Bayern Munich), Leroy Sane (Manchester City).
Washambuliaji: Mario Gomez (Stuttgart), Thomas Muller (Bayern Munich), Nils Petersen (SC Freiburg), Marco Reus (Borussia Dortmund), Timo Werner (RB Leipzig).
Mexico (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Guillermo Ochoa (Standard Liege), Alfredo Talavera (Toluca), Jesus Corona (Cruz Azul).
Mabeki: Carlos Salcedo (Eintracht Frankfurt), Nestor Araujo (Santos Laguna), Diego Reyes (Porto), Hector Moreno (Real Sociedad), Hugo Ayala (Tigres), Oswaldo Alanis (Guadalajara), Edson Alvarez (America), Jesus Gallardo (Pumas), Miguel Layun (Sevilla).
Viungo wa kati: Jesus Molina (Monterrey), Rafael Marquez (Atlas), Hector Herrera (Porto), Jonathan Dos Santos (LA Galaxy), Andres Guardado (Real Betis), Erick Gutierrez (Pachuca), Marco Fabian (Eintracht Frankfurt), Giovani Dos Santos (LA Galaxy).
Washambuliaji: Javier Hernandez (West Ham), Raul Jimenez (Benfica), Oribe Peralta (America), Jesus Manuel Corona (Porto), Carlos Vela (Los Angeles FC), Javier Aquino (Tigres), Hirving Lozano (PSV Eindhoven), Jurgen Damm (Tigres).
Sweden
Walinda lango: Robin Olsen (Copenhagen), Karl-Johan Johnsson (Guingamp), Kristoffer Nordfeldt (Swansea).
Mabeki: Mikael Lustig (Celtic), Victor Lindelof (Manchester United), Andreas Granqvist (Krasnador), Martin Olsson (Swansea), Ludwig Augustinsson (Werder Bremen), Filip Helander, Emil Krafth (both Bologna), Pontus Jansson (Leeds United).
Viungo wa kati: Sebastian Larsson (Hull), Albin Ekdal (Hamburg), Emil Forsberg (RB Leipzig), Gustav Svensson (Seattle Sounders), Oscar Hiljemark (Genoa), Viktor Claesson (Krasnador), Marcus Rohden (Crotone), Jimmy Durmaz (Toulouse).
Washambuliaji: Marcus Berg (Al Ain), John Guidetti (Alaves), Ola Toivonen (Toulouse), Isaac Kiese Thelin (Waasland-Beveren).
Korea Kusini (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Kim Seung-gyu (Vissel Kobe), Kim Jin-hyeon (Cerezo Osaka), Cho Hyeon-woo (Daegu FC).
Mabeki: Kim Young-gwon (Guangzhou Evergrande), Jang Hyun-soo (Tokyo FC), Jeong Seung-hyeon (Sagan Tosu), Yun Yeong-seon (Seongnam FC), Kwon Kyung-won (Tianjin Quanjian), Oh Ban-suk (Jeju Utd), Kim Jin-su (Jeonbuk Hyundai), Kim Min-woo (Sangju Sangmu), Park Joo-ho (Ulsan Hyundai), Hong Chul (Sangju Sangmu), Go Yo-han (FC Seoul), Lee Yong (Jeonbuk Hyundai).
Viungo wa kati: Ki Sung-yueng (Swansea City), Jeong Woo-young (Vissel Kobe), Kwon Chang-hoon (Dijon FCO), Ju Se-jong (Asan Mugunghwa), Koo Ja-cheol (Augsburg), Lee Jae-sung (Jeonbuk Hyundai), Lee Seung-woo (Hellas Verona), Moon Sun-min (Incheon Utd), Lee Chung-yong (Crystal Palace).
Washambuliaji: Kim Shin-wook (Jeonbuk Hyundai), Son Heung-min (Tottenham), Hwang Hee-chan (Red Bull Salzburg), Lee Keun-ho (Gangwon FC).

Kundi G

Ubelgiji
Kikosi bado hakijatajwa
Panama (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Jose Calderon (Chorrillo), Jaime Penedo (Dinamo Bucharest), Alex Rodriguez (San Francisco).
Mabeki: Azmahar Ariano (Patriots), Felipe Baloy (Municipal CSD), Harold Cummings (San Jose Earthquakes), Eric Davis (Dunajska Streda), Fidel Escobar (New York Red Bulls), Adolfo Machado (Houston Dynamo), Michael Murillo (New York Red Bulls), Luis Ovalle (Olimpia), Francisco Palacios (San Francisco), Richard Peralta (Alliance), Roman Torres (Seattle Sounders).
Viungo wa kati: Ricardo Avila (Gent), Edgar Barcenas (Cafetaleros de Tapachula), Ricardo Buitrago (Municipal), Miguel Camargo (Universidad San Martin), Adalberto Carrasquilla (Tauro), Armando Cooper (Universidad de Chile), Anibal Godoy (San Jose Earthquakes), Gabriel Gomez (Bucaramanga), Jose Gonzalez (Union Comercio), Cristian Martinez (Columbus Crew), Valentin Pimentel (Plaza Amador), Alberto Quintero (Universitario), Jose Luis Rodriguez (Gent).
Washambuliaji: Abdiel Arroyo (Alajuelense), Rolando Blackburn (Chorrillo), Ismael Diaz (Deportivo La Coruna), Jose Fajardo (Independiente), Roberto Nurse (Mineros Zacatecas), Blas Perez (Municipal), Luis Tejada (Sports Boys), Gabriel Torres (CD Huachipato).
Tunisia (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Aymen Mathlouthi (Al-Baten), Moez Ben Cherifia (ES Tunis), Farouk Ben Mustapha (Al-Shabab), Moez Hassen (Chateauroux).
Mabeki: Rami Bedoui (ES Sahel), Yohan Benalouane (Leicester), Syam Ben Youssef (Kasimpasa), Dylan Bronn (Gent), Khalil Chammam (ES Tunis), Oussama Haddadi (Dijon) , Ali Maaloul (Al-Ahly), Yassine Meriah (CS Sfaxien), Hamdi Nagguez (Zamalek), Bilel Mohsni (Dundee United).
Viungo wa kati: Mohamed Amine Ben Amor (Etoile du Sahel), Sai-Eddine Khaoui (Troyes), Ahmed Khalil (African Club), Ellyes Skhiri (Montpellier), Ferjani Sassi (Al-Nasr), Ghaylene Chaalali (ES Tunis), Mohamed Wael Larbi (Tours), Karim Laribi (Cesena).
Washambuliaji: Anice Badri (ES Tunis), Fakhreddine Ben Youssef (Al-Ittifaq), Naim Sliti (Dijon), Bassem Srarfi (Nice), Ahmed Akaichi (Al-Ittihad), Wahbi Khazri (Rennes), Saber Khalifa (African Club).
England
Walinda lango: Jack Butland (Stoke), Jordan Pickford (Everton), Nick Pope (Burnley).
Mabeki: Trent Alexander-Arnold (Liverpool), Gary Cahill (Chelsea), Fabian Delph (Manchester City), Phil Jones (Manchester United), Harry Maguire (Leicester), Danny Rose (Tottenham), John Stones (Manchester City), Kieran Trippier (Tottenham), Kyle Walker (Manchester City), Ashley Young (Manchester United).
Viungo wa kati: Dele Alli, Eric Dier (both Tottenham), Jordan Henderson (Liverpool), Jesse Lingard (Manchester United), Ruben Loftus-Cheek (Chelsea).
Washambuliaji: Harry Kane (Tottenham), Marcus Rashford (Manchester United), Raheem Sterling (Manchester City), Jamie Vardy (Leicester), Danny Welbeck (Arsenal).

Kundi H

Poland (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: Bartosz Bialkowski (Ipswich), Lukasz Fabianski (Swansea City), Lukasz Skorupski (Roma), Wojciech Szczesny (Juventus).
Mabeki: Jan Bednarek (Southampton), Bartosz Bereszynski (Sampdoria), Thiago Cionek (SPAL), Kamil Glik (Monaco), Artur Jedrzejczyk (Legia Warsaw), Marcin Kaminski (Stuttgart), Tomasz Kedziora (Dynamo Kyiv), Michal Pazdan (Legia Warsaw), Lukasz Piszczek (Borussia Dortmund).
Viungo wa kati: Jakub Blaszczykowski (Wolfsburg), Pawel Dawidowicz (Palermo), Przemyslaw Frankowski (Jagiellonia Bialystok), Jacek Goralski (Ludogorets Razgrad), Kamil Grosicki (Hull City), Damian Kadzior (Gornik Zabrze), Grzegorz Krychowiak (Paris St-Germain), Rafal Kurzawa (Gornik Zabrze), Karol Linetty (Sampdoria), Maciej Makuszewski (Lech Poznan), Krzysztof Maczynski (Legia Warsaw), Slawomir Peszko (Lechnia Gdansk), Maciej Rybus (Lokomotiv Moscow), Sebastian Szymanski (Legia Warsaw), Piotr Zielinski (Napoli), Szymon Zurkowski (Gornik Zabrze).
Washambuliaji: Dawid Kownacki (Sampdoria), Robert Lewandowski (Bayern Munich), Arkadiusz Milik (Napoli), Krzysztof Piatek (Cracovia), Lukasz Teodorczyk (Anderlecht), Kamil Wilczek (Brondby).
Senegal
Walinda lango: Khadim Ndiaye (Horoya AC), Abdoulaye Diallo (Rennes), Alfred Gomis (Torino)
Mabeki: Kara Mbodji (Anderlecht), Kalidou Koulibaly (Napoli), Moussa Wague (Eupen), Saliou Ciss (Angers), Youssouf Sabaly (Bordeaux), Lamine Gassama (Alanyaspor), Armand Traore (Nottingham Forest), Salif Sane (Hannover 96)
Viungo wa kati: Pape Alioune Ndiaye (Stoke), Idrissa Gueye (Everton), Cheikhou Kouyate (West Ham), Cheikh N'Doye (Birmingham)
Washambuliaji: Sadio Mane (Liverpool), Diao Balde Keita (Monaco), Ismaila Sarr (Rennes), Diafra Sakho (Rennes), Moussa Konate (Amiens), Mame Biram Diouf (Stoke), Mbaye Niang (AC Milan)
Colombia (Kikosi kamili cha wachezaji 23 kuthibitishwa baadaye)
Walinda lango: David Ospina (Arsenal), Camilo Vargas (Deportivo Cali), Ivan Arboleda (Banfield), Jose Fernando Cuadrado (Once Caldas).
Mabeki: Cristian Zapata (Milan), Davinson Sanchez (Tottenham), Santiago Arias (PSV Eindhoven), Oscar Murillo (Pachuca), Frank Fabra (Boca Juniors), Johan Mojica (Girona), Yerry Mina (Barcelona), William Tesillo (Santa Fe), Bernardo Espinosa (Girona), Stefan Medina (Monterrey), Farid Díaz (Olimpia).
Viungo wa kati: Wílmar Barrios (Boca Juniors), Carlos Sánchez (Espanyol), Jefferson Lerma (Levante), Jose Izquierdo (Brighton), James Rodriguez (Bayern Munich), Giovanni Moreno (Shanghai Shenhua), Abel Aguilar (Deportivo Cali), Mateus Uribe (America), Yimmi Chara (Junior), Juan Fernando Quintero (River Plate), Edwin Cardona (Boca Juniors), Juan Cuadrado (Juventus), Gustavo Cuellar (Flamengo), Sebastian Perez (Boca Juniors).
Forwards: Radamel Falcao (Monaco), Duvan Zapata (Sampdoria), Miguel Borja (Palmeiras), Carlos Bacca (Villarreal), Luis Fernando Muriel (Sevilla), Teofilo Gutierrez (Junior).
Japan
Kikosi bado hakijatangazwa

Utatazama harusi ya kifalme au fainali kati ya Chelsea na Manchester United kesho Jumamosi

$
0
0



Haki miliki ya pichaGetty Images
Image caption Mwanamfalme Prince William atakosa kuhudhuria fainali ya kesho kusimamia harusi ya nduguye Prince Harry.
Je wewe utafutilia harusi ya kifalme ambayo itafanyika keshi Jumamosi kati mwanamfalme Prince Harry na Meghan Markle au utatazama mechi ambayo ni fainali ya mechi ya FA kati ya mahasimu Chelsea na Manchester United.
Mwanamfalme Prince William atakosa kuhudhuria fainali hiyo ya kesho Jumamosi kwa kuwa ndiyo siku ya harusi ya nduguye Prince Harry.
Prince William atakuwa msimamizi wa harusi ya nduguye huko Windsor kesho Jumamosi.
William amekuwa rais wa FA tangu mwaka 2006 na mara nyingi ndiye hupeana vikombe na medali.
Mjane wa Ray Wilkins Jackie atatoa kombe hilo kwa washindi huko Wembley.
"Prince William hatahudhuria fainali ya FA kutokana na majukumu kama msimamizi wa harusu ya ndugu yake," alisema msemaji wa Kensington Palace.
Msemaji wa FA alisema: "Tunawatakia Prince William na wale watafunga ndoa siku njema."
Ray Wilkins ambaye alifariki mwezi uliopita akiwa miaka 61, alishinda kombe la FA kama mchezaji wa Manchester United mwaka 1983 na kufunga wakati wa fainali.
Pia alishinda kombe hilo mara tatu akiwa meneja wa Chelsea.

ada zinazohusiana

Viewing all 21576 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>